VR Technology.

VR Technology.

Ifahamu teknolojia ya Virtual Reality (VR) inayotikisa ulimwengu kwa sasa.
Kama wewe ni mmoja wa watu wanaofuatilia mambo ya teknolojia na habari utakuwa sio mgeni sana na huu msamiati unaotajwa kila kukicha katika mitandao na vyombo vya habari.
Virtual Reality au VR kama inavyotamkwa na watu wengi imepata umaarufu sana katika miaka ya hivi karibuni tofauti na ukongwe wa teknolojia hii.
Kampuni ya Nintendo ya Japani ndio ilikuwa kampuni ya kwanza kuleta teknolojia hii katika uso wa dunia katika miaka ya 70. Haikupata umaarufu mkubwa japo iliendelea kutumika katika maeneo mengi hasa ya elimu ya urubani na upasuaji.
Wanafunzi walioukuwa wakichukua mafunzo ya urubani katika vyuo mbali mbali walitumia VR ili kupata radha au muonekano ule ule uliokuwa katika mzingira halisi. Wanafunzi wa masuala ya uuguzi na udaktari pia wametumia sana teknolojia hii katika mafunzo yao.
Kwa sasa hali imekuwa tofauti kabisa, lengo la wanasayansi kuifanya teknolojia hii kuwa sehemu ya burudani linaonekana kufanikiwa kwa kiasi kikubwa sana. Kwa sasa VR inatumika katika majumba ya sinema, sehemu za kucheza magemu na katika burudani nyingine nyingi.
VR ni nini hasa?
Hii ni teknolojia inayohusisha kuvaa kisanduku kilicho na matundu mawili usawa wa macho, kupitia matundu hayo unaweza ukaangalia muvi, kucheza magemu na mambo mengine mengi kama ukiwa katika ulimwengu halisi. Kupitia VR unaweza ukatembelea jangwa la Sahara, kuvuka mito mikubwa, kupambana na majitu ya ajabu. Kwa kifupi VR ni teknolojia inayokuwezesha kuota ndoto zako ukiwa macho.
Hayo yote yanawezeshwa na kompyuta au simu yenye uwezo wa kuzalisha picha zinazoonekana katika kisanduku hicho. Facebook wameifanya teknolojia hii kupata umaarufu tena kwa kuachia visanduku vya VR vijulikanavyo kama Oculus ambavyo kwa sasa vinatumika sana.  Kampuni za Sonny, Google na Samsung nao wameungana na Facebook katika hili.
Faida za Virtual Reality
VR zinafaida nyingi katika ulimwengu wa sasa ila hapa nitajaribu kuelezea chache kati ya hizo.
Elimu; Majeshi na vyuo mbalimbali vimekuwa vikitumia teknolojia hii muda sasa katika kufundishia hasa masomo yanayohitaji mazoezi ya kutosha na ya hatari.
Gaming ; Wapenda magemu wamepata teknolojia sahihi katika kuleta msisimko wa mchezo kwa kushiriki moja kwa moja katika mchezo husika. Fikiria unakimbizana na Usain Bolt katika mbio za mita 100 ndani ya VR.
Design ; Kupitia VR wasanifu majengo wanapata kazi rahisi ya kujua nini wataenda kufanya kabla hata ya kitu chenyewe kukamilika.
Porn: Asilimia 35 ya internet ni ngono, nadhani hapa umeelewa.
Hasara za VR
Kwa kiasi kikubwa teknolojia hii inamadhara sana katika mahusiano ya mtu na mtu, fikiria mpo kwenye ukumbi na wote mmevaa visanduku vya VR.  Au upo kwenye daladala huku unajisanduku cha VR usoni.
Nini kifanyike?
Kwa matumizi ya kielimu na burudani VR ni kitu kizuri sana, ila inapaswa watu wafahamu kwa undani teknolojia hii kabla ya kuanza kuitumia. Pia kwa watoto hasa wanaosoma ni vizuri kuwapa maelezo mazuri kabla ya kuwanunulia vifaa hivi.
Share on Google Plus

About mboo safi nene na ndefu

0 comments:

Post a Comment